12/15/10

Utu wa Nyani



Katika mji wa Bangalore huko India. Watu wawili vipofu walitaka kunywa maji katika bomba lakini hawakuweza kulifungua bomba, akaja huyu Nyani na kuwafungulia bomba na kuwapa ruhusa ya kunywa maji baada ya kumaliza kunywa maji wakaondoka huyu nyani akanywa na yeye kisha akalifunga bomba kabla ya kuondoka katika eneo hilo.

Huu ni uthibitisho mkubwa kwamba ubinadamu gani upo - hata sisi binadamu siku hizi hatuna utu kama anavyo huyu Nyani...

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Hakika ni kweli kabisa nakubali ya kwamba nyani ana utu kuliko hata sisi binadamu. Ahsante kwa hili!!

Simon Kitururu said...

Hii kali!