5/23/15

MAJI NA JUISI YA LIMAO ASUBUHI NI KINGA TOSHA YA MWILI
1. Huongeza Kinga yako ya mwili hasa kupambana na magonjwa madogo kama mafua, na kikohozi kutokana na kuwa na vitamin C 2. Husafisha Mfumo wako wa chakula, kuondoa sumu mwilini na kuzuia tumbo kujaa gesi mara kwa mara 3. Huleta hewa safi kinywani. Ni Muhimu sana kwa watu wanaonuka midomo 4. Hukuongezea uchangamfu na kufanya siku yako ianze vizuri sana 5. Husaidia majeraha kupona kwa haraka kutokana na kuwa na ascorbic acid ya kutosha. Pia huimarisha mifupa 6. Husaidia mmeng’enyo wa chakula utakachokula asubuhi au mchana kwa kuondoa vikwazo vyote vinavyoweza kuzuia umeng’enyaji wa chakula. 7. Huimarisha Ngozi yako, kuondoa makunyanzi na kukupa muonekano mzuri. 8. Husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uzito kwani maji moto ya limao huyeyusha mafuta ya kutosha. 9. Huyapa macho yako afya nzuri na kuimarisha kuona. 10. Huondoa hali ya kuhitaji kahawa kila asubuhi ambayo si nzuri kiafya.

No comments: